Pata taarifa kuu
AMISOM-SIASA-SOMALIA-UN

Kikosi cha AMISOM kupunguzwa nchini Somalia

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema wanajeshi 1,000 watapunguzwa kutoka kwenye kikosi cha wanajeshi zaidi ya 20,000 wa kulinda amani  nchini Somalia maarufu kama AMISOM, licha ya mashambulizi kuongezeka mjini Mogadishu.

Wanajeshi wa AMISOM nchini Somalia
Wanajeshi wa AMISOM nchini Somalia TOBIN JONES / AU UN IST / AFP
Matangazo ya kibiashara

Pendekezo hili liliwasilishwa na Uingereza na kuungwa mkono na wajumbe wote katika Baraza hilo lakini ikaamuliwa kuwa kikosi hicho cha AMISOM kitaendelea na operesheni zake nchini Somali kwa mwaka mmoja zaidi.

Hata hivyo, maafisa wa polisi 1,040 kutoka mataifa mbalimbali ya Sierra Leon, Nigeria na Ghana hawatapunguzwa.

Tangu mwaka 2017, kumekuwa na mpango wa kuwapunguza wanajeshi wa AMISOM na taratibu kuanza kukabidhi ulinzi wa nchi hiyo kwa vikosi vya Somalia.

AMISOM iliundwa la Baraza la Usalama la Umoja wa Afrika mwaka 2007 na kuidhinishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwenda kulinda serikali ya Mogadishu inayotambuliwa kimataifa, lakini pia kuzuia mashambulizi ya kundi la Boko Haram.  .

Mataifa ya Afrika yanayounda jeshi la AMISOM ni pamoja na Uganda ambayo ina idadi kubwa ya wanajeshi zaidi ya 6,000  Burundi, Ethiopia, Kenya na Djibouti.

Jeshi la AMISOM,  limepiga kambi Kusini na katikati ya nchi hiyo.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.