MONUSCO: Tuko tayari kusaidia katika mchakao wa uchaguzi
Wananchi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, sasa wanatarajiwa kupiga kura siku ya Jumapili Desemba 30, kumchagua rais mpya na viongozi wengine.
Imechapishwa:
Uchaguzi huo ambao umesubiriwa tangu mwaka 2006, ulitarajiwa kufanyika Jumapili iliyopita lakini ukaahirishwa kwa wiki moja zaidi ili Tume ya Uchaguzi imemalize maandalaizi yake.
Wagombea wa urais, wameingia katika wiki ya mwisho ya kutafuta kura, wakati huu Umoja wa Mataifa ukisema kuwa utakuwa tayari kusaidia, ili kufanikisha zoezi hili.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesema ucheleweshwaji huu utasaidia kuweka mazingira ya Uchaguzi huo kuwa huru na haki.