Pata taarifa kuu
NIGERIA-USALAMA

Wachimba migodi 16 watekwa nyara kaskazini mwa Nigeria

Wachimba migodi kumi na sita wametekwa nyara na kundi la wahalifu kaskazini mwa Nigeria, katika eneo linalojulikana kwa visa hivyo ambapo watekaji nyara wamekuwa wakiomba fidia kwa familia za mateka , polisi na wakuu wa eneo hilo wamesema.

Maafisa wa usalama wakipiga doria karibu na eneo ambapo watu wenye silaha walimteka mhadhiri wa Arkeoloji kutoka Ujerumani Peter Breunig na mwenzake Johannes Behringer katika kijiji cha Janjala, Nigeria, Februari 24, 2017.
Maafisa wa usalama wakipiga doria karibu na eneo ambapo watu wenye silaha walimteka mhadhiri wa Arkeoloji kutoka Ujerumani Peter Breunig na mwenzake Johannes Behringer katika kijiji cha Janjala, Nigeria, Februari 24, 2017. © AP
Matangazo ya kibiashara

Watu hao walitekwa Jumanne usiku walipo kuwa njiani wakirudi kutoka mgodini katika eneo la Birnin Gwari katika Jimbo la Kaduna, msemaji wa polisi Yakubu Sabo amesema.

"Wachimba migodi 16 walikuwa wakisafiri kwa lori wakati walipovamiwa karibu na kijiji cha Bogoma na kundi la wahalifu ambao waliwapeleka mahali pasipojulikana," amesema.

"Wanaume wetu kutoka kitengo cha kupambana na utekaji nyara wamekuwa wakitumika eneo hilo ili kupata na kuokoa mateka."

Kwa mujibu wa Abdullahi Bature, msemaji wa kiongozi wa jadi wa Birnin Gwari, Zubairu Mai-Gwari, kisa hicho cha utekaji nyara kilitokea wakati gari waliokuwemo ilikuwa imeegesh akando ya barabara baada ya kupatwa na tatizo.

"Walitekwa nyara usiku lakini watu watatu miongoni mwa wachimba migodi hao walifaulu kutimka wakati walikuwa wakipelekwa katika kichaka. Watekaji nyara hao wanataka fidia," Bature amesema, akiongeza kuwa watekaji nyara hao waliwasiliana na familia za mateka wakiomba pesa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.