Ethiopia: Watu 18 wapoteza maisha katika ajali ya helikopta ya kijeshi
Watu kumi na nane wamepotza maishakatika ajali ya helikopta ya kijeshi iliyotokea leo Alhamisi Agosti 30 katika mkoa wa Oromo, kusini mwa mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, televisheni Fana BC imeripoti kwenye tovuti yake.
Imechapishwa:
Watu wote waliokua ndani ya helikopta hiyo, wajeshi 15 na raia wa kawaida watatu, wamepoteza maisha katika ajali hiyo.
"Helikopta hiyo, ambayo ilikuwa ya Wizara ya Ulinzi, ilianguka wakati ilikua ikijaribu kupaa angani kutoka Dire Dawa, kaskazini-magharibi mwa Ethiopia, kwenda Bishoftu (kilomita 40 kusini-mashariki mwa Addis Ababa) na ilikua na watu 18 ", televisheni Fana BC imeripoti, bila hata hivyo kutoa taarifa yoyote kuhusu sababu za ajali ya helikopta hiyo.
Helicopter crashes in Ethiopia, killing 18 people https://t.co/0RmFSubw7q pic.twitter.com/jyGEXx41qH
FANA BROADCASTING C (@fanatelevision) August 30, 2018
Mnamo mwaka 2013, ndege ya mizigo ya kijeshi ya Ethiopia ilianguka wakati ilipokua ikitua kwenye uwanja wa ndege wa Mogadishu nchini Somalia, na kuua watu wanne kati ya sita waliokuemo.