Pata taarifa kuu
CAMEROON-SIASA-BIYA

Msafara wa Waziri wa Ulinzi wa Cameroon washambuliwa

Msafara wa magari uliokuwa unamsafirisha Waziri wa Ulinzi wa Cameroon Joseph Beti Assomo umeshambuliwa katika eneo ambalo kuna wazungumzaji wa lugha ya Kiingereza.

Wanajeshi  wa Cameroon wakiwa katika eneo linalotaka kujitenga
Wanajeshi wa Cameroon wakiwa katika eneo linalotaka kujitenga REUTERS/Joe Penney
Matangazo ya kibiashara

Ripoti zinasema kuwa, wanajeshi wanne walijeruhiwa huku washambuliaji kadhaa wakiuawa.

Hili ni shambulizi linalokuja, baada ya rais Paul Biya mwenye umri wa miaka 85 kutangaza kuwa atawania tena urais wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba.

Kwa muda mrefu sasa, wanaharakati kutoka Kusini mwa nchi hiyo wamekuwa wakishinikiza kujitenga na kuunda taifa lao wanalotaka liitwe Ambazonia.

Hata hivyo, serikali ya Yaounde imeendelea kusisitiza kuwa, Kusini mwa nchi hiyo ni Cameroon na madai ya wanaharakati hayo hayawezi kupewa nafasi.

Maelfu ya raia wa Cameroon wanaozungumza Kiingereza wamekimbilia nchini Nigeria kwa wasiwasi wa kuuwawa kutokana na makabiliano kati ya maafisa wa usalama na wanaharakati.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.