ZIMBABWE-AFRIKA KUSINI-NYAMA
Zimbabwe yapiga marufuku vyakula vya nyama kutoka Afrika Kusini
Zimbabwe inaungana na mataifa mengine kupiga marufuku kuingizwa kwa vyakula vya nyama kutoka nchini Afrika Kusini.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Hatua hii inakuja baada ya kuzuka kwa maambukizi ya backteria ya listeria vilivyobainika katika vyakula hivyo ambavyo ni hatari kwa matumizi ya binadamu.
Serikali ya Afrika Kusini imepiga marufuku uuzwaji wa sausage inayofahamika kama Polony, na kutoa wito kwa watu kutokula bidhaa hiyo.
Ripoti zinasema kuwa watu 180 wamepoteza maisha kwa kula bidhaa hiyo iliyokuwa na sumu.
Wamiliki wa maduka yanayouza Sausage hizo, wamelazimika kuziondoa baada ya tangazo hilo.