Viongozi wa ECOWAS walaani mashambulizi ya kigaidi nchini Burkina Faso
Marais wa Togo na Niger wamezuru jijini Ouagadougou nchini Burkina Faso kusimama na wananchi wa taifa hilo baada ya kundi la kijihadi kushambulia Ubalozi wa Ufaransa na Makao makuu ya jeshi iliyopita.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Mashambulizi hayo yaliyotekelezwa na kundi la GSIM, yalisababisha vifo vya wanajeshi nane na wengine kujeruhiwa.
Rais wa Togo Faure Gnassingbe ambaYe ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS, amesema mataifa hayo yataendelea kushirikiana kwa lengo la kushinda ugaidi Afrika Magharibi.
Naye rais wa Niger Mahamadou Issoufou ambaye ni rais wa nchi za Sahel zinazojumuisha, Burkina Faso, Niger, Mauritania, Chad na Mali, amesema vikosi vya nchi hizi vitaendelea kushirikiana na Ufaransa ili kushinda ugaidi.
Burkina Faso inasema inaendelea kuchunguza namna shambulizi hilo lilivyofanyika, wakati huu rais Roch Marc Christian Kabore akisema itachukua muda mrefu kushinda ugaidi nchini humo.