Pata taarifa kuu
DRC-SIASA-MAANDAMANO-CENCO

Waandaji wa maandamano dhidi ya rais Kabila kukamatwa

Chanzo kutoka Mahakamani nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kimesema hati ya kukamatwa kwa waandaaji wa maandamano kumshinikiza rais Joseph Kabila kuodoka madarakani, imetolewa.

Maandamano yaliyopita jijini Kinshasa dhidi ya rais Joseph Kabila
Maandamano yaliyopita jijini Kinshasa dhidi ya rais Joseph Kabila REUTERS/Thomas Mukoya
Matangazo ya kibiashara

Kwa mujibu wa chanzo hicho, watu ambao wanaolengwa kukamatwa ni wanachama wa kamati iliyo karibu na Kanisa Katoliki, ambayo imetangaza maandamano mapya siku ya Jumapili.

Shirika la Habari la Ufaransa AFP, linaripoti kuwa atu watano na ambao ni washirika wa karibu wa maaskofu pamoja na maaskofu wakuu wa Kanisa Katoliki wanapangwa kukamatwa.

Serikali ya rais Kabila, imewashtumu Maaskofu wa Kanisa Katoliki kwa kuendelea kuchochea hali ya kisiasa nchini humo huku Maaskofu hao wakisema hawatarudi nyuma katika juhudi zao za kumtaka rais Kabila kuondoka madarakani na kutowania urais mwisho wa mwaka huu.

Mbali na maandamano hayo yanayopangwa na Maaskofu wa Kanisa Katoliki, wanasiasa wa upinzani wanaomuunga mkono Waziri Mkuu Bruno Tshibala, nao wameandaa maandamano Jumapili hii, kuunga mkono mchakato wa kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwezi Desemba.

Haijafahamika iwapo, rais Kabila ambaye ameongoza madarakani mwaka 2001 hatawania urais baada ya muhula wake kumalizika.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.