Pata taarifa kuu
LIBYA-MAPIGANO-USALAMA

Watu wasiopungua 20 wauawa katika mapigano Libya

Mapigano makali yaliyozuka katika uwanja wa ndege jijini Tripoli jana kati ya waasi na jeshi la serikali, yamesababisha vifo vya watu 20. Ndege tano zimeathiriwa na mapigano hayo, kwa mujibu wa maafisa wa usalama.

Ofisi za uwanja wa ndege wa Mitiga,Tripoli, zikiwa hazina watu kufuatia mapigano Jumatatu, Januari 15, 2018.
Ofisi za uwanja wa ndege wa Mitiga,Tripoli, zikiwa hazina watu kufuatia mapigano Jumatatu, Januari 15, 2018. REUTERS/Ismail Zitouny
Matangazo ya kibiashara

Serikali nchini Libya, inasema mapigano hayo yalianza baada ya waasi kujaribu kuvamia gereza moja wakiwa na lengo la kuwasadia wenzao kutoroka.

“Shambulio hilo ni jaribio la kundi moja la wapiganaji kuachiliwa kwa wafuasi wake waliokuwa wakishikiliwa na kundi wanalopingana nalo,” Serikali ya Libya inayotambuliwa na jumuiya ya kimataifa imesema.

Mapigano haya yaliyotokea yalihusisha makundi ya wanamgambo hasimu katika mji mkuu wa Libya, Tripoli

Haya ndio mapigano mabaya zaidi kuwahi kuripotiwa jijini Tripoli katika miezi ya hivi karibuni na kusabbaisba uwanja huo wa ndege wa kimataifa kufungwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.