Pata taarifa kuu
RSF-WANAHABARI

RSF: Jumla ya waandishi wa habari 65 wameuawa mwaka 2017

Waandishi wa habari 65 na wafanyakazi wa vyombo vya habari wameuawa katika mwaka 2017, hii ni kwa mujibu wa ripoti iliyochapishwa na shirika la wanahabari wasio na mipaka RSF.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye moja ya harakati za kuripoti matukio kwenye eneo la Israel na Palestina
Waandishi wa habari wakiwa kwenye moja ya harakati za kuripoti matukio kwenye eneo la Israel na Palestina REUTERS/Mohamad Torokman
Matangazo ya kibiashara

Miongoni mwao 50 walikuwa ni maripota, hii ikiwa ni idadi ndogo zaidi katika kipindi cha miaka 14.

Hata hivyo ripoti inasema kuwa huenda kupungua kwa idadi ya vifo vya wanahabari imetokana na waandishi na ripota wengi kuacha kuripoti habari kwenye maeneo yenye vita.

Nchi ya Syria ambao kwa zaidi ya miaka 6 imeshuhudia vita vya wenywe kwa wenyewe, imesalia kuwa nchi hatari zaidi kwa waandishi wa habari kufanya kazi, imeonesha ripiti ya RSF ambayo imesema waandishi wa habari 12 waliuawa nchini humo, ikifuatiwa na Mexico ambako 11 waliuawa.

Miongoni mwa waliouawa nchini Mexico ni mwanahabari maarufu wa habari za biashara haramu ya dawa za kulevya nchini humo Javier Valdez ambaye mauaji yake yalitamausha wengi.

Waandamanaji nchini Kenya wakiwarushia mawe polisi na waandishi wa habari, waliokuwa wakiripoti maandamano ya kupinga vitendo vya rushwa, Nairobi, 3 Novemba, 2016.
Waandamanaji nchini Kenya wakiwarushia mawe polisi na waandishi wa habari, waliokuwa wakiripoti maandamano ya kupinga vitendo vya rushwa, Nairobi, 3 Novemba, 2016. REUTERS/Thomas Mukoya

Mwandishi mwingine wa habari wa shirika la AFP aliuawa kwa kupigwa risasi nchini Mexico katika mji wa Kaskazini wa Sinaloa.

Nchi ya Ufilipino imekuwa ni taifa jingine hatari kwenye ukanda wa Asia kwa waandishi wa habari kufanya kazi ambapo ripiti inaonesha waandishi wa habari watano waliuawa kwa kupigwa risasi mwaka uliopita.

Ongezeko hili lilitokana na matamshi ya rais Rodrigo Duterte ambaye alisema “haimaanishi ukiwa muandishi wa habari basi ndio usiuawe ikiwa unajihusisha na biashara haramu”.

Hata hivyo hakukuwa na mwanahabari aliyeuawa mwaka uliotangulia nchini Ufilipino.

Waandishi wa habari nchini Misri wakiwa wamebeba kamera zao nje ya ofisi ya chama cha waandishi wa habari
Waandishi wa habari nchini Misri wakiwa wamebeba kamera zao nje ya ofisi ya chama cha waandishi wa habari Reuters

Kiujumla ripoti ya RSF inasema kuwa idadi ya vifo vya wanataaluma wa habari imepungua kidunia katika kipindi cha miaka 14.

Katika vifo vya wanahabari 65, ripoti inaonesha kuwa wanahabari 39 waliuawa huku wengine wakipoteza maisha wakiwa kwenye majukumu yao ya kazi kama vile mashambulizi ya anga au yale ya kujitoa muhanga.

RSF inasema kuwa huenda pia vifo vimepungua kutokana na waandishi wengi wa habari kutopokea mafunzo ya kujilinda wakati wa vita.

Nchi ya Uturuki inatajwa kwenye ripoti hii kwa kuwa na magereza mengi ambayo waandishi wa habari wanashikiliwa, ambapo kwa sasa zaidi ya wanahabari 42 wanazuiliwa.

Nchi nyingine zinazofunga waandishi wa habari kwenye jela zake ni pamoja na Syria ambako kuna wanahabari 24, Iran wapo 23 na Vietnam ambako wako 19.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.