Pata taarifa kuu
TOGO-MAANDAMANO-USALAMA

Mamia ya raia wa Togo wakimbilia Ghana

Mamia ya raia wa Togo wamekimbilia nchi jirani ya Ghana kwa kuhofia kukamatwa na maafisa wa serikali. Hali ya wasi wasi inaendelea kuripotiwa nchini humo

Upinzani unatazamia kuingia mitaani kwa maandamano makubwa, kushinikiza mabadiliko ya Katiba na kumalizika kwa uongozi wa rais Faure Gnassingbe
Upinzani unatazamia kuingia mitaani kwa maandamano makubwa, kushinikiza mabadiliko ya Katiba na kumalizika kwa uongozi wa rais Faure Gnassingbe Anne Cantener/RFI
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii imekuja kwa sababu ya maandamano yanayoendelea hasa jijini Lome, kushinikiza mabadiliko ya Katiba na kumalizika kwa uongozi wa rais Faure Gnassingbe.

Maandamano wa upinzani yanatarajiwa kuendelea leo na mengine yanatarajiwa kufanyika kesho.

Upinzani umtuhumu rais Faure Gnassingbe na Serikali yake kwa kupindisha kweli na kukwepa uhalisia wa wito wanaoutoa kuhusu kufanyika kwa mabadiliko ya katiba ya nchi hiyo.

Muungano huu wa vyama 14 vya upinzani unataka kuwepo kwa mihula miwili ya rais na kuwekwa kwa mifumo miwili ya upigaji kura.

Upinzani umeitisha maandamano makubwa ya nchi nzima kushinikiza kuondoka madarakani kwa Serikali ya rais Gnassingbe.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.