Polisi yamshikilia mwanasiasa mwengine wa upinzani Zambia
Polisi nchini Zambia wanamshikilia kiongozi mmoja wa chama kidogo cha upinzani cha United Progressive Party (UPP) Savior Chishimba, ambaye ameonekana kuwa mkosoaji numba mbili wa Rais Edgar Lungu.
Imechapishwa:
Bw Chishimba alikamatwa siku ya Alhamisi punde baada ya kukamilishwa mahojiano ya moja kwa moja kwenye studio ya kituo cha televisheni binafsi mjini Lusaka.
Huyu atakuwa ni mpinzani wa pili kukamatwa baada ya kinara wa upinzani nchini humo Hakainde Hichilema, hatua inayochukuliwa na wanaharakati kuwa ni njama za kutaka kuuminya upinzani nchini humo.
Hivi karibu Hichilema alisema kwa kipindi chote hicho amekuwa akipitia kipindi kigumu kwa sababu haki zake msingi zinakiukwa na amezuiwa katika mazingira mabaya.
Hichilema alikamatwa mapema mwaka huu baada ya msafara wake kuzuia msafara wa rais Edgar Lungu.
Mwanasiasa huyo ameyakanusha madai hayo na kusema ni ya kisiasa yanayotumiwa dhidi yake.